Tetesi za soka : Man City na Barca wafanya mazungumzo juu ya Haaland
Chanzo cha picha
Manchester City na Barcelona wafanya mazungumzo juu ya mshambuliaji Erling Haaland, kiungo wa kati wa West Ham Mateus Fernandes anafuatliwa na Manchester United, Newcastle wanammezea kiungo wa Monaco Lamine Camara.
Barcelona wamefanya mazungumzo na Manchester City kuhakikisha wanapata fursa ya kumsajili mshambuliaji wa Norway Erling Haaland, 25, iwapo atapatikana kwa uhamisho. (Sport - in Spanish)
Hata hivyo, mwakilishi wa Haaland, Rafaela Pimenta, alipuuza uvumi unaomhusisha kiungo huyo na Barcelona kwenye kipindi cha televisheni cha Uhispania. (Times - subscription required)

Kiungo wa kati wa Newcastle United na Italia Sandro Tonali, 25, yuko kwenye orodha ya wanaolengwa na Manchester United ya wachezaji kiungo wa kati wanaoweza kufuatiluwa. (Sun)
No comments
Note: only a member of this blog may post a comment.