Tetesi za soka : Rashford anaweza kurejea Man Utd
Chanzo cha picha,
Marcus Rashford anaweza kurudi Manchester United msimu huu wa joto, Tottenham wanatafuta mchezaji wa kuchukua nafasi ya Igor Tudor na Arsenal wanaandaa mkataba na Leon Goretzka.
Mshambuliaji wa Uingereza Marcus Rashford, 28, anaweza kurudi Manchester United baada ya muda wake wa mkopo Barcelona, ambao wanamtaka winga wa Chelsea na Ureno Pedro Neto, 26, kama mbadala. (Mundo Deportivo - in Spanish)
Rashford anataka kubaki Barca, lakini mazungumzo yamegonga mwamba na mkurugenzi wa michezo Deco amependekeza msimu mwingine wa mkopo ili kuwapa timu hiyo ya Uhispania muda zaidi wa kulipa ada ya chaguo la kumnunua kutoka kwa Manchester United. (Talksport)

Tottenham wanaandaa chaguzi zinazowezekana za kuchukua nafasi ya Igor Tudor kama kocha mkuu ikiwa wataamua kufanya mabadiliko mengine ya usimamizi. (Athletic - subscription required)
No comments
Note: only a member of this blog may post a comment.