
Mshambuliaji wa Liverpool Diogo Jota amefariki katika ajali ya barabarani akiwa na umri wa miaka 28.
Kaka yake mshambuliaji huyo wa Ureno Andre Silva pia alifariki katika ajali hiyo iliyotokea katika jimbo la Zamora nchini Uhispania.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 pia alikuwa mchezaji wa kulipwa, wa klabu ya daraja la pili ya Ureno ya Penafiel.
Gazeti la Guardia Civil limeiambia BBC Michezo kuwa Jota na kaka yake walifariki saa sita usiku siku ya Alhamisi saa za Uhispania.
Gari lao aina ya Lamborghini, liliacha njia baada ya tairi kulipuka na kuwaka moto.