Poshy Queen Afunguka Jinsi Ndoa Ilivyombadilisha na Kumpa Utulivu wa Maisha
Poshy Queen Afunguka Jinsi Ndoa Ilivyombadilisha na Kumpa Utulivu wa Maisha
0 amesema maisha yake yamebadilika kwa kiasi kikubwa baada ya kuingia kwenye ndoa, akieleza kuwa sasa anaishi kwa utulivu zaidi kuliko ilivyokuwa zamani.
Akizungumza na Mwanaspoti, Poshy Queen alisema ndoa imempa amani ya moyo na kumfanya ajikite zaidi kwenye maisha yake binafsi badala ya kelele za mitandaoni.
"Kila hatua ya maisha ina wakati wake. Kwa sasa nimetulia sana tofauti na zamani. Ndoa imenifanya niwe na amani zaidi," amesema Poshy Queen.
Poshy Queen aliwahi kuwa gumzo kubwa alipokuwa kwenye mahusiano na 1, lakini baada ya kuachana alianza kupunguza uwepo wake kwenye mitandao ya kijamii.
Baadaye alithibitisha kuwa ameolewa na mwanaume anayejihusisha na shughuli za udalali, hatua iliyowashangaza wengi lakini pia kuonyesha kuwa ameanza ukurasa mpya wa maisha.
Kwa sasa, Poshy Queen anaendelea na biashara zake huku akifurahia maisha ya utulivu, faragha na amani zaidi kuliko ilivyokuwa zamani.


No comments
Note: only a member of this blog may post a comment.