Tetesi za Soka Ulaya Jumatatu: Wilson akubali mkataba mpya wa West Ham
Chanzo cha picha
Callum Wilson akubali kusalia West Ham, Ibrahim Sangare aongezwa kwenye orodha ya wanaowindwa na Manchester United na Manchester City yakaribia kumsajili Tino Livramento.
Mshambuliaji wa Uingereza Callum Wilson, 34, amekubali mkataba mpya wa mwaka mmoja na West Ham wiki chache tu baada ya kuonekana kuwa mwenye kuondoka hivi karibu. (Telegraph - subscription required)

Manchester United imemuongeza kiungo wa Nottingham Forest wa Ivory Coast Ibrahim Sangare, 28, kwenye orodha ya wachezaji inaowataka wajiunge nao msimu huu wa joto. (CaughtOffside)

Manchester City inakaribia kumsajili beki wa pembeni wa Newcastle United, Tino Livramento, 23. (Football Insider)
No comments
Note: only a member of this blog may post a comment.