Tetesi za Soka Ulaya: Camavinga kuondoka Madrid, Arsenal yaanza mazungumzo na Lukeba
Chanzo cha picha,
Vilabu kadhaa vya Ligi Kuu England vimefunguliwa milango ya matumaini ya kumsajili kiungo wa kimataifa wa Ufaransa Eduardo Camavinga, 23, baada ya Real Madrid kuwa tayari kusikiliza ofa kwa ajili yake dirisha la majira ya kiangazi. (Marca)
Arsenal wameanza mazungumzo na RB Leipzig kuhusu kumsajili beki wa kati wa Ufaransa Castello Lukeba, 23. (L'Equipe)
Chelsea, Liverpool na Manchester United zinatarajiwa kupambana kusaka saini ya kiungo wa Crystal Palace na England Adam Wharton, 22. (Football Insider)
Chelsea na Manchester United pia zinatajwa kuwa katika ushindani mwingine wa uhamisho, huku zote zikiwa miongoni mwa vilabu vinavyomtaka mshambuliaji wa Ujerumani mwenye umri wa miaka 19 Said El Mala kutoka 1. FC Köln. (Caughtoffside)
No comments
Note: only a member of this blog may post a comment.