-->

Breaking News

Tetesi za Soka Ulaya: Arsenal yamtaka Goretzka wa Bayern

 lChanzo cha picha,

Maelezo ya picha,Mchezaji wa kimataifa wa Ujerumani, Leon Goretzka

Arsenal itakabiliwa na ushindani kutoka Juventus katika kusaini mkataba na mchezaji wa kimataifa wa Ujerumani, Leon Goretzka huku kiungo huyo mwenye umri wa miaka 31 akitarajiwa kuondoka Bayern Munich mkataba wake utakapoisha msimu huu wa joto. (Gazzetta dello Sport)

AC Milan wanamtazama mshambuliaji wa Jamhuri ya Ireland, Troy Parrott wakati wa kiangazi huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 akiwa na thamani ya takriban pauni milioni 25 kutoka AZ Alkmaar. (Independent)

Brighton wana hamu ya kukamilisha mkataba na Cologne kwa winga wa Ujerumani mwenye umri wa miaka 19 Said el Mala baada ya mchezaji huyo kubadilisha mawakala. (Bild)

No comments

Note: only a member of this blog may post a comment.

🔔 Enable Notifications

Get latest songs and entertainment updates instantly.