Tetesi za soka Jumatano: Arsenal wanamtaka Brandt

Arsenal wana shauku ya kumsajili kiungo wa kati wa Ujerumani Julian Brandt, 29, mkataba wake wa Borussia Dortmund utakapomalizika msimu huu wa joto. (Metro),
Manchester United, Arsenal na Chelsea zote zina nia ya kumsajili kiungo wa kati wa Freiburg, Johan Manzambi, 20, kutoka Uswizi. (Teamtalk)
Hata hivyo, Arsenal wameachana na nia ya kumsajili kiungo wa kati wa Italia wa Newcastle, Sandro Tonali, 25. (Chronicle)

Kurudi Serie A pia kunaonekana kutokuwa rahisi kwa Tonali baada ya Newcastle kuweka bei ya pauni milioni 77 (euro 90) kwa mchezaji huyo, ambayo itaifanya Juventus ishindwe, lakini Manchester United na Manchester City bado wana nia naye. (Matteo Moretto )
No comments
Note: only a member of this blog may post a comment.