Tetesi za soka Alhamisi:Man Utd yammezea mate Murillo
Chanzo cha picha,
Beki wa Nottingham Forest na Brazil, Murillo, mwenye umri wa miaka 23, ni mmoja wa mabeki kadhaa walio kwenye orodha fupi ya Manchester United ya wachezaji wanaoweza kusajiliwa msimu huu wa joto. (i paper)
Arsenal itafikiria ofa ya kumnunua beki wa Newcastle na Uingereza, Tino Livramento msimu huu wa joto, huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 bado hajaonesha nia ya kuongeza mkataba wake zaidi ya 2028. (Telegraph)
Tottenham Hotspur itamruhusu mlinda lango Antonin Kinsky, mwenye umri wa miaka 22, kuondoka klabuni hapo kwa mkopo msimu huu wa joto ili kujenga upya kujiamini kwake baada ya mchezaji huyo wa kimataifa wa Jamhuri ya Czech kuondolewa baada ya dakika 17 pekee dhidi ya Atletico Madrid siku ya Jumanne. (Telegraph)
No comments
Note: only a member of this blog may post a comment.