Marcus Rashford: Galasa United, dhahabu Barcelona
Marcus Rashford, ambaye amekuwa kama mgeni asiyehitajika Old Trafford tangu mwisho wa mwaka jana, yuko karibu zaidi na ndoto ya kuhamia Nou Camp baada ya makubaliano ya awali kufikiwa.
Hii si habari ya kushangaza sana, kwani Rashford anaripotiwa kuwa na hamu ya muda mrefu ya kujiunga na miamba hao wa Hispania, na mwezi uliopita alitamka wazi kuwa anatamani kucheza pamoja na nyota kinda Lamine Yamal.
Barcelona pia hawajaficha nia yao. Mwezi Mei, mkurugenzi wa michezo Deco alikiri kuwa wanampenda Rashford na kusema kuwa anaweza "kuboresha kikosi".
Hilo ndilo jambo linalozua mjadala kwa sasa, je, Rashford anaweza kweli kutoa mchango mkubwa kwa timu yake mpya?
No comments
Note: only a member of this blog may post a comment.