A Zeno.FM Station Tetesi za soka Ulaya Jioni hii: Harry Kane kutua Liverpool? anataka kurejea EPL

Tetesi za soka Ulaya Jioni hii: Harry Kane kutua Liverpool? anataka kurejea EPL


a

Chanzo cha picha,Getty Images

Mshambuliji wa Bayern Munich Harry Kane, 31, anafikiria kurejea Uingereza msimu huu wa kiangazi, huku Liverpool ikiwa ni mahali anapopendelea zaidi. (Fichajes - in Spanish)

Chelsea lazima walipe Manchester United pauni milioni 5 ikiwa watachagua kupinga kugeuza mkopo wa mshambuliaji wa Uingereza Jadon Sancho kuwa mkataba wa kudumu. (Subscriotion is required)

Tottenham wameanza kuchunguza mpango wa kumnunua kiungo wa kati wa Southampton mwenye umri wa chini ya miaka 21 wa Southampton, Tyler Dibling. (Givemesport)

f

Chanzo cha picha,Getty Images

Maelezo ya picha,Isak

Mshambuliaji wa Newcastle Alexander Isak yuko tayari kuhamia Barcelona lakini angependelea kujiunga na Liverpool ikiwa watamnunua mchezaji huyo wa kimataifa wa Sweden mwenye umri wa miaka 25 msimu huu. (El Nacional - in Spanish)

Kiungo wa kati wa Ubelgiji Kevin De Bruyne, 33, amefanya mazungumzo na klabu ya MLS San Diego kuhusu uhamisho wa bila malipo mkataba wake Manchester City utakapokamilika msimu huu wa kiangazi. (Sun)

Tags :-

Post a Comment

0 Comments