🎤 Davido Kutumbuiza FIFA World Cup 2026 Countdown Concert Los Angeles
🎤 Davido Kutumbuiza FIFA World Cup 2026 Countdown Concert Los Angeles
Mkali wa Afrobeat kutoka Nigeria, Davido, anatarajiwa kuwa mmoja wa wasanii wakuu watakaotumbuiza katika tamasha la FIFA World Cup 2026 Countdown Concert litakalofanyika Juni 10 ndani ya Crypto.com Arena jijini Los Angeles, Marekani.
Tamasha hilo maalum limeandaliwa ikiwa ni sehemu ya kuhesabu siku kuelekea kuanza rasmi kwa Kombe la Dunia 2026 ambalo litafanyika katika nchi tatu za Marekani, Canada na Mexico.
🔥 Davido na Major Lazer Jukwaa Moja
Davido atapanda jukwaani sambamba na kundi maarufu la muziki la Major Lazer linaloongozwa na DJ na mtayarishaji mashuhuri duniani, Diplo.
⚽ FIFA Yaandaa Tamasha Kubwa
Kwa mujibu wa waandaaji, tamasha hilo litaanza saa 5:00 usiku kwa saa za Los Angeles na linatarajiwa kuvuta maelfu ya mashabiki wa soka na muziki kutoka sehemu mbalimbali duniani.
FIFA pia imeeleza kuwa majina zaidi ya wasanii wa kimataifa yatatangazwa katika siku zijazo kabla ya hafla hiyo kufanyika.
🏆 Kombe la Dunia 2026 Kuanza Juni 11
Kombe la Dunia 2026 litafunguliwa rasmi Juni 11, 2026 na kwa mara ya kwanza katika historia litafanyika katika nchi tatu tofauti ambazo ni Marekani, Canada na Mexico.
Michuano hiyo itamalizika Julai 19, 2026 ambapo mchezo wa fainali utachezwa New Jersey nchini Marekani.
🌟 Shakira, BTS na Madonna Watajwa
Taarifa zinaeleza kuwa show ya fainali ya Kombe la Dunia 2026 huenda ikapambwa na mastaa wakubwa duniani akiwemo Shakira, BTS, Madonna pamoja na majina mengine makubwa kutoka tasnia ya muziki duniani.
Wasanii wengine wanaotajwa kupewa nafasi ya kutumbuiza katika matukio ya Kombe la Dunia ni pamoja na Rema, Tyla, Future na Katy Perry.
No comments
Note: only a member of this blog may post a comment.