💰 Phyna Ajutia Kutumia Fedha za Big Brother Naija Kuwasaidia Ndugu
💰 Phyna Ajutia Kutumia Fedha za Big Brother Naija Kuwasaidia Ndugu
Mshindi wa msimu wa saba wa Big Brother Naija, Josephina Ijeoma Otabor maarufu kama Phyna amesema anajutia namna alivyotumia fedha zake baada ya kushinda shindano hilo mwaka 2022.
Phyna aliibuka mshindi wa BBNaija Season 7 na kuondoka na zawadi ya Naira milioni 100 lakini sasa amesema hakufanya maamuzi sahihi ya kifedha kipindi hicho.
😔 Phyna Akiri Kutokuwekeza
Nyota huyo amesema wakati anapata fedha hizo alikuwa bado mdogo na hakuwahi kushika fedha nyingi kabla jambo lililomfanya kushindwa kuwekeza vizuri.
Badala ya kuwekeza kwenye biashara, Phyna amesema alitumia fedha nyingi kuwasaidia ndugu pamoja na familia yake.
👨👩👧 Ndugu Zake Wamgeuka
Phyna amesema kinachomuuma zaidi ni namna baadhi ya ndugu zake walivyokuwa wakimuomba msaada wa kifedha bila kumpa ushauri wa namna ya kutunza fedha zake.
Amedai kuwa baada ya fedha kuisha wengi wao walimgeuka na kumuacha akipambana mwenyewe.
📈 Mashabiki Watoa Ushauri
Kauli ya Phyna imezua mjadala mkubwa mitandaoni huku mashabiki wengi wakisema ni funzo kwa vijana wanaopata mafanikio ya haraka bila mipango ya kifedha.
Wengine wamemtaka kutumia umaarufu wake kuanza upya kupitia biashara pamoja na mikataba ya matangazo.
No comments
Note: only a member of this blog may post a comment.