Kiwanja cha Jumba la Davido Chafikia Thamani ya Sh15.2 Bilioni
Kiwanja cha Jumba la Davido Chafikia Thamani ya Sh15.2 Bilioni
Msanii maarufu wa Nigeria, Davido, ameendelea kuonyesha mafanikio makubwa baada ya kushiriki maendeleo ya ujenzi wa jumba lake jipya la kifahari lililopo eneo la Eko Atlantic nchini Nigeria.
Kupitia video na picha zilizosambaa mtandaoni, Davido alionyesha baadhi ya maeneo muhimu yatakayokuwemo ndani ya nyumba hiyo ikiwemo studio ya kisasa ya muziki, klabu mbili za burudani pamoja na vyumba binafsi kwa ajili ya watoto wake wote.
“Watoto wangu wote watakuwa na vyumba vyao binafsi pamoja na sehemu maalum za burudani ndani ya nyumba.”
Thamani ya Kiwanja Yapanda Maradufu
Davido ameeleza kuwa alinunua kiwanja hicho kwa takribani Naira bilioni 4, lakini kwa sasa thamani yake imeongezeka hadi karibu Naira bilioni 8, sawa na zaidi ya Sh15.2 bilioni.
Eneo la Eko Atlantic limekuwa moja ya maeneo ya kifahari zaidi nchini Nigeria ambapo mastaa, wafanyabiashara wakubwa na watu maarufu huwekeza kwenye majumba ya kisasa yenye hadhi ya juu.

No comments
Note: only a member of this blog may post a comment.