-->

Breaking News

Tetesi za soka Ulaya: Bayern, Arsenal 'zatoana roho' kwa Anthony Gordon

 dChanzo cha picha,

Bayern Munich wameonyesha nia ya kumsajili mshambuliaji wa Newcastle United na England, Anthony Gordon, mwenye miaka 25, ambaye pia anafuatiliwa na Arsenal (Caughtoffside).

Manchester United wanatarajia kutumia uhusiano ulioko ndani ya kikosi cha England kuwazidi kete Manchester City katika mbio za kumsajili kiungo wa Nottingham Forest, Elliot Anderson, mwenye miaka 23 (Teamtalk).

Liverpool wanamfuatilia winga wa Brighton & Hove Albion na Gambia, Yankuba Minteh, mwenye miaka 21, aliyewahi kufanya kazi chini ya Arne Slot huko Feyenoord, kama mbadala wa mshambuliaji wa Misri, Mohamed Salah, anayeondoka mwishoni mwa msimu (Mirror).

s

Chanzo cha picha,Getty Images

Maelezo ya picha,Yankuba Minteh

Arsenal na Manchester City wameungana na Aston Villa katika mbio za kumsajili beki wa Real Betis, Oscar Mingueza, mwenye miaka 26 (Teamtalk).

mziki mpya Tanzania

nyimbo mpya 2026

bongo flava mpya

habari za wasanii leo

matokeo ya mechi leo

simba vs yanga

No comments

Note: only a member of this blog may post a comment.

🔔 Enable Notifications

Get latest songs and entertainment updates instantly.