Tetesi za soka Ulaya: Arsenal kusajili beki wawili, Martinelli kuondoka
Chanzo cha picha,
Arsenal wanatafuta kuimarisha safu ya ulinzi msimu huu wa joto, huku wakilenga kumsajili beki wa Real Madrid, Victor Valdepenas (19), pamoja na beki wa kati wa Como na timu ya vijana ya Hispania chini ya miaka 21, Jacobo Ramon (21). (CaughtOffside)
Winga wa Brazil Gabriel Martinelli (24) anasisitiza kubaki Arsenal licha ya dalili kutoka klabuni kuwa anaweza kuuzwa msimu huu wa joto. (Football Insider)
Borussia Dortmund wanafikiria kufanya jaribio la tatu kumsajili winga wa England, Jadon Sancho (26), ambaye kwa sasa yuko kwa mkopo huko Aston Villa na anatarajiwa kuondoka Manchester United kama mchezaji huru msimu huu wa joto. (Telegraph)
Tottenham Hotspur wanataka kumsajili kipa wa Manchester City na timu ya taifa ya England, James Trafford (23), kama sehemu ya mipango yao ya dirisha kubwa la usajili. (Teamtalk)
No comments
Note: only a member of this blog may post a comment.