Tetesi za soka Ulaya: Zidane kuinoa Ufaransa, De Zerbi kutua Spurs
Chanzo cha picha,
Kocha wa zamani wa Real Madrid, Zinedine Zidane, amekubali kuwa kocha wa timu ya taifa ya Ufaransa baada ya kumalizika kwa fainali za Kombe la Dunia mwaka huu. Zidane, mwenye miaka 53, anatarajiwa kuchukua nafasi ya Didier Deschamps (ESPN).
Kocha wa zamani wa Brighton & Hove Albion na Marseille, Roberto De Zerbi, yuko tayari kuwa kocha mkuu wa kudumu wa Tottenham Hotspur iwapo klabu hiyo itasalia Lgi kuu ya England (Telegraph).
Winga wa Manchester United na England Jadon Sancho, ambaye kwa sasa yuko kwa mkopo Aston Villa, amefanya mazungumzo na Borussia Dortmund kuhusu uwezekano wa kurejea Bundasliga kwa uhamisho wa bure, huku mchezaji huyo mwenye miaka 25 akiwa tayari kupunguza mshahara wake (Sky Sports Deutschland).
Manchester United inamtaka beki wa kushoto Alphonso Davies kutoka Bayern Munich, huku klabu hiyo ya Bundesliga ikiwa tayari kusikiliza ofa kwa ajli ya mchezaji huyo mwenye miaka 25 (CFBayerninsider).
No comments
Note: only a member of this blog may post a comment.