Tetesi za soka Ulaya: Tonali kuzitosa Man Utd, Man City kwenda Italia
Chanzo cha picha,
Manchester City na Manchester United wanavutiwa na kiungo wa Newcastle, Sandro Tonali, 25, lakini mchezaji huyo wa zamani wa AC Milan anapendelea kurejea nyumbani Italia (Talksport).
Ben White, mlinzi wa Arsenal mwenye umri wa 28 anaweza kuondoka msimu huu huku Everton wakionesha hamu ya kumsajili (FourFourTwo).
Aston Villa ni miongoni mwa klabu kadhaa za Ligi kuu England zinazoangalia uwezekano wa kumsajili mshambuliaji wa Paris St-Germain kutoka Senegal, Ibrahim Mbaye, mwenye umri wa 18, msimu huu (Sky Sports).
Manchester United wamemuweka nyota wa Fulham na Marekani, Antonee Robinson, mwenye umri wa 28, kwenye orodha yao ya mabeki wa kushoto wanaohitajika msimu huu (Football Insider).
No comments
Note: only a member of this blog may post a comment.