-->

Breaking News

Tetesi za soka Ulaya: Man United inamtaka Lewis-Skelly wa Arsenal

 sChanzo cha picha,

Manchester United wanapanga mpango wa kushangaza wa kumsajili beki wa kushoto wa Arsenal, Myles Lewis-Skelly, huku msingi wa mkataba tayari ukiwa umewekwa kwa mchezaji huyo wa taifa la England mwenye umri wa miaka 19. (Teamtalk)

Kiungo wa Manchester City, Bernardo Silva, 31, anapendelea kuhamia Barcelona mkataba wake utakapomalizika, lakini mchezaji huyo Mreno ana wasiwasi kuhusu uwepo wa nyota wengi wadogo wenye kasi kwenye kikosi cha Barcelona. (Sport)

Kiungo wa Newcastle, Bruno Guimaraes, 28, yupo kwenye orodha ya juu ya Manchester United kama mbadala wa Mbrazil mwenzake Casemiro, 34, na klabu hiyo tayari imefanya mazungumzo na mawakala wake. (UOL)

Mshambuliaji mkongwe wa Poland, Robert Lewandowski, 37, anaangalia kama atasaini mkataba wa mwaka mmoja kuendelea kusalia Barcelona au kuhamia klabu nyingine, pengine katika ligi ya Marekani, MLS. (Fabrizio Romano)

No comments

Note: only a member of this blog may post a comment.

🔔 Enable Notifications

Get latest songs and entertainment updates instantly.