Tetesi za Soka Ulaya Jumanne: Juve wanamtaka Spence wa Tottenham
Chanzo cha picha,
Djed Spence wa Tottenham anatarajiwa kuichezea Juventus, Real Madrid yamweka Mauricio Pochettino kwenye orodha ya watakaowania nafasi ya ukocha, Liverpool yafikiria kumsajili winga wa Ufaransa Moussa Diaby.
Juventus wana nia ya kumsajili beki wa pembeni wa Tottenham na Uingereza Djed Spence, 25, msimu huu wa joto (Gazzetta dello Sport - in Italian)

Liverpool wanafikiria kumsajili winga wa Al-Ittihad na Ufaransa Moussa Diaby, mwenye umri wa miaka 26, huku mchezaji huyo wa zamani wa Aston Villa akitaka kuondoka katika klabu hiyo ya Saudi Pro League msimu huu wa joto. (Teamtalk)

Newcastle wameazimia kumshikilia kiungo wa kati Bruno Guimaraes, 28, na wanafanya mazungumzo ya mkataba na mchezaji huyo wa kimataifa wa Brazil licha ya Manchester United kuonyesha nia ya kutaka kumsajili. (Caughtoffside)
No comments
Note: only a member of this blog may post a comment.