Tetesi za soka Ulaya Ijumaa: Real Madrid na Man United zampigania Bruno Guimaraes.
Chanzo cha picha,
Manchester United wako kwenye mazungumzo ya kiwango cha juu kumsajili nahodha wa Newcastle United Bruno Guimaraes kwa takriban pauni milioni 69, lakini nia mpya kutoka kwa Real Madrid inatishia kutatiza uhamisho wa kiungo huyo wa kati wa Brazil mwenye umri wa miaka 28. (Reuters)
Hatahivyo, Magpies wana nia ya kuendelea na Guimaraes na wanapanga mazungumzo kuhusu mkataba unaoweza kuweka rekodi mpya katika klabu hiyo. (TeamTalks)
Manchester United itakataa juhudi za Barcelona za kuongeza mkopo wa mchezaji wa kimataifa wa Uingereza Marcus Rashford, 28, kwa msimu mwingine, ikiambia klabu hiyo ya Uhispania kulipa £26m iliyokubaliwa hapo awali au kumrudisha fowadi huyo Old Trafford. (Mirror)
Real Madrid wako kwenye mazungumzo na beki wao wa miaka 33 wa Ujerumani Antonio Rudiger kuhusu mkataba mpya. (Marca)
No comments
Note: only a member of this blog may post a comment.