Tetesi za soka Ulaya: Arsenal yamtaka Franca
Chanzo cha picha,
Arsenal wameongeza juhudi za kusaka beki wa kulia, huku nyota wa Roma mwenye umri wa miaka 22 Wesley Franca akitajwa kuwa chaguo lao kuu. (Teamtalk)
Liverpool wanaongoza mbio za kumsajili kiungo wa Real Madrid Eduardo Camavinga, mbele ya Chelsea, baada ya kufanya mazungumzo mara mbili na wawakilishi wake. (Caught Offside)
Kocha wa Barcelona Hansi Flick amesema hana uhakika kuhusu mustakabali wa Marcus Rashford, ambaye yupo kwa mkopo akitokea Manchester United, huku klabu hiyo ikiwa na chaguo la kumsajili kwa pauni milioni 26. (Manchester Evening News)
Arsenal wako na presha kubwa ya kuuza wachezaji katika dirisha la majira ya joto, huku wachezaji wachache tu wakichukuliwa kuwa hawagusiki. (Telegraph)
No comments
Note: only a member of this blog may post a comment.