Tetesi za soka Ulaya Alhamisi: Marcus Rashford kusalia Barcelona kwa mkopo
Chanzo cha picha,
Barcelona itajaribu kumbakisha mshambuliaji wa Manchester United Marcus Rashford, 28, kwa mkopo kwa msimu mwingine ili kuepuka kulipa ada ya uhamisho ya £26m. (Daily Mail)
United inaweza kumnunua kiungo wa kati wa Nigeria Wilfred Ndidi, 29, kutoka Besiktas, huku mlinda lango wa Uturuki Altay Bayindir, 27, akielekea upande mwingine. (SporX - In Turkish)
Borussia Dortmund wanaamini kuwa wanaweza kumshawishi Jadon Sancho, 25, wa United kusaini kwa mara ya tatu katika klabu hiyo ya Bundesliga. (Times - Subscription Required)

Manchester United wana nia ya wazi ya kumnunua kiungo wa kati wa Italia Sandro Tonali lakini Newcastle United itadai ada ya zaidi ya £100m ikiwa wataamua kumuuza mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25. (I)
No comments
Note: only a member of this blog may post a comment.