Tetesi za soka Ulaya: Al-Ittihad warejea kwa Mo Salah
Chanzo cha picha,
Al-Ittihad walikataliwa ofa yao ya £150m kwa ajili ya mshambuliaji wa Liverpool Mohamed Salah mwaka 2023, lakini klabu hiyo ya Saudi Pro League imefufua nia yao upya ya kumsajili nyota huyo wa Misri mwenye umri wa miaka 33, ambaye atapatikana bure baada ya kuondoka Liverpool mwishoni mwa msimu huu wa kiangazi (ESPN).
Salah hakupata ofa kutoka klabu zingine kama ilivyotarajia katika dirisha la Januari, na katika mazungumzo ya kuondoka msimu huu, wamiliki wa Liverpool Fenway Sports Group waliona kuendelea kung'ang'ania ili kupata ada kungeongeza mzozo (Telegraph).
Liverpool wamekuwa wakiwasiliana mara kwa mara na kocha wa zamani wa Real Madrid, Xabi Alonso, ambaye aliwahi kushinda ligi ya mabingwa akiwa mchezaji wa klabu hiyo, na Mhispania huyo yuko tayari kuchukua nafasi ya Arne Slot msimu huu iwapo masharti fulani yatatimizwa (Bild).
Liverpool wamehusishwa na winga wa Ufaransa Michael Olise kama mrithi wa Salah, lakini Bayern Munich hawana haraka kuhusu mustakabali wa mchezaji huyo mwenye miaka 24 kwani ana mkataba hadi 2029 na hana kipengele cha kuuzwa (Sport Bild).
No comments
Note: only a member of this blog may post a comment.