Tetesi za soka Jumamosi: Newcastle United yamfuatilia Liam Delap
Chanzo cha picha,
Mshambuliaji wa Chelsea Liam Delap anawindwa na Newcastle msimu huu wa joto huku ada ya takriban pauni milioni 40 ikitangazwa kwa Muingereza huyo mwenye umri wa miaka 23. (Talksport)
Kiungo wa kati wa Manchester United Kobbie Mainoo, 20, anatarajiwa kuongeza mkataba wake hadi mwaka 2031 na kuongeza mara nne mshahara wake Old Trafford hadi pauni 120,000 kwa wiki, pamoja. (Talksport)
Matumaini ya Liverpool ya kuishawishi Inter Milan kumuuza mlinzi wa kimataifa wa Italia Alessandro Bastoni, 26, yanafifia. (Teamtalk)

Tottenham wamemtazama mlinda lango wa Ujerumani Noah Atubolu, 23, huku nambari moja wa sasa Guglielmo Vicario akiangalia kurejea Italia akiwa na wachezaji wanaopigiwa upatu na Inter Milan. (Mail)
No comments
Note: only a member of this blog may post a comment.