'Alinidunga na sindano iliyokuwa na virusi vya HIV baada ya kukataa kuolewa naye'
Chanzo cha picha
Tukio la kushangaza limetokea jimbo la Telangana nchini India, baada ya mwanaume mmoja aliyekuwa amejawa na hasira kumdunga sindano iliyo na damu mwanamke mmoja aliyekataa kuoleka na yeye.
Sindano hiyo ilikuwa imebeba damu iliyokuwa na virusi vya HIV.
Polisi wa eneo hilo wanasema mwanamke huyo kwa sasa anapokea matibabu.
Kulingana na polisi miezi michache iliyopita, familia ya mwanamke wa miaka 24 wanaoishi eneo la Annojiguda nje ya mji wa Hyderabad, na familia moja ya kijana mwenye umri wa miaka 25 ambao walikuwa majirani, walikuwa wamekubali kuwaoza wawili hao. Familia hizi ni jamaa moja.
No comments
Note: only a member of this blog may post a comment.