Simba kurejea Tanzania leo, Yafunga mahesabu hivi
Kikosi cha Simba kimehitimisha pre-season nchini Misri ambapo leo timu inatarajiwa kurejea nchini kuhitimisha awamu ya mwisho ya maandalizi
Kocha Mkuu wa Simba Fadlu Davids amepata takribani wiki nne kukiandaa kikosi chake kambi ikianzia mji wa Ismailia na kisha kuhitimishwa Cairo
Sehemu kubwa ya wachezaji wamepata wa kutosha wa maandalizi ukiondoa wachezaji wachache ambao walichelewa kutokana na changamoto za vibali huku kiungo Neo Maema akitua baada ya kumaliza majukumu ya kuitumikia timu ya Taifa ya Afrika Kusini kwenye michuano ya CHAN 2024
Baada ya kurejea nchini Simba itakuwa na wiki moja zaidi ya kujiandaa kabla ya Tamasha la Simba Day litakalofanyika Septemba 10
Mnyama atakuwa siku nyingine chache za kujiandaa kabla ya mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Yanga ambao mpaka sasa ratiba inaonyesha utapigwa Septemba 16
Baadae Simba itaelekea Botswana kwenye mchezo wa mkondo wa kwanza hatua ya awali ligi ya mabingwa dhidi ya Gaborone United utakaopigwa Septemba 20
.jpeg)
No comments
Note: only a member of this blog may post a comment.