
Real Madrid pia wanavutiwa na mlinzi wa Ufaransa William Saliba, 24, ambaye ni anacheza na Gabriel kama walinzi wa kati katika klabu ya Arsenal. (Mirror)
Arsenal wanajiandaa kumpa Gabriel, 27, mkataba mpya ili kuzuia kunyakuliwa kwa beki huyo wa kati wa Brazil kutoka Saudi Arabia. (Football Insider)
The Gunners, kwa upande wake, wameungana na Liverpool katika mbio za kumsajili mlinzi wa Uholanzi Jorrel Hato mwenye umri wa miaka 19 kutoka Ajax. (Team talk)
Atalanta wameweka bei ya pauni milioni 50 kwa mshambuliaji Ademola Lookman, 27, huku Manchester United na Newcastle United zikiwa na nia ya kumpata. (Tutomercato)