Liverpool wanatazamiwa kuzishinda Chelsea na Newcastle United katika usajili wa majira ya kiangazi wa Marc Guehi wa Crystal Palace, 24, huku Anfield ndio mahali anapopendelea mlinzi huyo wa Uingereza. (Mirror)
Wakala wa mshambuliaji wa Argentina Julian Alvarez anasema Liverpool ilimtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 kabla ya kujiunga na Atletico Madrid kutoka Manchester City msimu uliopita. (Winwin via Liverpool Echo)
Liverpool wanaweza kufikiria kumuuza mshambuliaji wa Uruguay Darwin Nunez msimu wa joto, huku meneja wa Arsenal Mikel Arteta akiaminika kumtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25. (Fichajes)
Real Madrid itafanya jaribio la kumnunua beki wa Arsenal Mfaransa William Saliba, 23, msimu wa joto. (Relevo)