-->

Breaking News

Mpenzi mpya wa Rihanna ni bilionea wa Toyota


Mapema wiki hii picha zinazomwonyesha mwanamuziki Rihanna akiwa ndani ya bwawa la kuogelea na mwanamume wa Kiarabu zilizagaa mitandaoni.Hatimaye Rihanna ametoka hadharani na mwanamume huyo na ametambulika kuwa ni bilionea wa magari ya Toyota nchini Saudia Arabia, Hassan Jameel.
Mwanamume huyo ni makamu wa Rais wa Kampuni ya familia yake iitwayo Abdul Latif Jameel Domestic ambayo imepewa leseni ya kuuza magari yanayotengenezwa na Kampuni ya Toyota nchini Saudi Arabia tangu mwaka 1955.Jarida la Forbes mwaka jana liliitaja familia ya Jameel kushika namba 15 katika orodha ya matajiri katika nchi za Mashariki ya Kati.
Tokeo la picha la rihanna and hassan jameel
jameel pia anamiliki ligi ya mpira wa miguu nchini Saudi Arabia maarufu kama Jameel League.Mwanamume huyo pia siyo mgeni katika viwanja vya watu maarufu nchini Marekani, mwaka jana aliwahi kutajwa kuwa ana uhusiano wa kimapenzi na mwanamitindo maarufu Naomi Campbell.
Rihanna kabla ya kutua kwa Mwarabu huyo amewahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na  rapa Drake naTravis Scott, mcheza kikapu Matt Kemp na mwimbaji waR&B,ChrisBrown.Tokeo la picha la rihanna and hassan jameel
Tokeo la picha la rihanna and hassan jameel

No comments

Note: only a member of this blog may post a comment.

🔔 Enable Notifications

Get latest songs and entertainment updates instantly.